Thursday, November 12, 2009

16 vyajitosa shindano la kielimu la Zain


Peter Edson
Vyuo vikuu 16 kutoka katika kila pande ya Tanzania jana vilijitokeza katika mchakato wa kuvipata vyuo vikuu vinne vitakavyoshiriki mashindano ya kielimu ya Zain Afrika nchini Uganda mwakani.

Kampuni ya simu za mkononi ya Zain Afrika imekuwa ikiandaa mashindano hayo kila mwaka, mwakani vyuo vikuu vinne kutoka katika nchi za Kenya, Tanzania, Uganda, Malawi, Zambia, Ghana, Sierra Leon na Nigeria ambayo mwaka jana ilitwa ushindi wa shindano hilo vitashiriki kwenye kinyang’anyiro hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini jana Meneja wa huduma za jamii katika kampuni hiyo Tunu Kavishe alivitaja vyuo vikuu vinavyoshiriki katika mchakato huo kuwa ni Chuo kikuu cha Ardhi, Hubert Kairuki Memorial, Mount Meru, Chuo kikuu cha Muhimbili na Mzumbe.

Vingine ni Chuo kikuu cha Sokoine, St Augustine, St John’s, Teofilo Kisanji, Chuo kikuu Huria, Chuo kikuu cha Tumaini-Moshi, chuo kikuu Arusha, Chuo kikuu Dar es salaam, Chuo kikuu Dodoma, chuo kikuu Zanzibar pamoja na chuo kikuu cha Serikali.
Alisema wanafunzi kutoka katika vyuo hivyo wameandaliwa vya kutosha kwani baada ya Tanzania kushindwa kutamba katika mashindano hayo wamegundua kuwa uelewa mdogo wa wanafunzi nchini ndiyo kikwazo cha kutofanya vizuri.

“Tumejitahidi kuwatafuta wanafunzi ambao tunaamini kuwa watafanya vizuri, tunaendelea na zoezi la kuwashindanisha ili kupata vyuo vikuu vine vitakavyoshiriki mwakani.

“Mara nyingi tumeshindwa kufanya vizuri, kinachotukwamisha ni wanafunzi wetu kutokuwa na uelewa wa kutosha wa mambo yanayojiri duniani, lakini kwa sasa tunaamini mafanikiop yapo,” alisema Kavishe.

Alisema wamepokea jumla ya wanafunzi 64 pamoja na walimu wao 32 kutoka katika vyuo hivyo 16 na kwamba kazi ya kuwashindanisha inaendelea vizuri.

Zain Afrika huandaa mashindano ya kielimu yajulikanayo kwa jina la Zain Africa Challenge kila mwaka na kuvihusisha vyuo vikuu kutoka katika nchi mbalimbali Afrika, washindi wa shindano hilo huzawadiwa dola za Kimarekani 5000 kila mmoja kwa wanafunzi 4, na chuo hupata dola 50,000.

Monday, October 26, 2009

TATEDO wawakumbuka watoto walemavu



Peter Edson


TAASISI isiyokuwa ya kiserikali ya TATEDO jana ilikabidhi msaada wa Oveni ya mkaa yenye thamani ya Sh 550,000/= kwenye kituo cha Manzese Day Care kinachojishughulisha na kuwalea watoto wenye ulemavu.

Akikabidhi msaada huo afisa habari wa TaTEDO Editha Mushi alisema taasisi hiyo imeamua kutoa msaada huo kwa wakinamama wanao wahudumia watoto walemavu kwa lengo la kuhakikisha kuwa watoto hao wanapata mahitaji salama na bora.

Alisema thamani ya Oveni inayotumia mkaa ni kiasi cha Sh 550,000 lakini pia kabla ya kuwakabidhi msaada huo waliendesha semina ya siku mbili na kutumia kiasi cha Sh 450,00 , semina elekezi iliyokuwa ikilenga kuwapatia ujuzi wa matumizi sahihi ya jiko hilo

“Tumetumia kiasi cha Sh 1milioni katika shughuli hii ya semina kwa wakinamama 20 pamoja na gharama za kutengeneza jiko hilo lenye uwezo wa kuoka mikate, keki na pamoja na kutumika katika shughuli ya kupika chakula cha aina zote”alisema Mushi.


Naye Mwenyekiti wa kikundi hicho cha wanawake kijulikanacho kwa jina la Manzese Day Care Mery Njoka, mbali na kushukuru kwa msaada huo alitoa wito kwa Serikali kuwa na mpango mkakati na wa muda mrefu wenye lengo la kuondoa fikra potofu iliyojengeka kuwa walemavu ni watu tegemezi

Alisema kituo hicho kina jumla ya walemavu 40 wakiwemo wenye mtindio wa ubongo, wenye vichwa vikubwa, wenye fistula pamoja na waliopinda miguuu.

“Kwa kweli sisi wenyewe hatuwezi kufanya jambo lolote bali tunaamini kuwa kupitia wadau mbalimbali tunaweza ,kufanikisha malengo yetu ya kuwalea watoto hawa walemavu” alisema Njoka.

Alisema pamoja na jitihada nzuri za Serikali zinazoonyesha kila dalili njema za kutaka kuwasaidia watoto walema na wasiojiweza baadhi ya taasisi binafsi zimekosa uaminifu kwa watoto wanaowalea,hivyo alitoa wito kwa taasisi hizo kutekeleza wajibu wao badala ya kuweka mbele maslahi yao kwanza.

Mwisho.

Wednesday, May 27, 2009

CCM poll victory confirms party’s hold on rural electorate



By Prince Pierre

Civic United Front (CUF) leader Prof Ibrahim Lipumba has argued that existing constitution and lack of voter education has played a role in the opposition’s defeat in recent polls in Busanda.

CCM has maintained its winning trend after defeating three opposition parties including Chadema an immediate opponent by a significant margin. The campaign was mainly marked by fierce rivalry between CCM and Chadema.

According to the party’s Publicity Secretary Capt. John Chiligati. CCM candidate’s victory is attributable to party’s rigorous move to implement its manifesto, a trend that transforms the lives of the poor.

However, scores of analysts who were reached for comments said that voters in rural areas could easily give in due to threats and ignorance over lack of civic education, although to a certain extent people might still be trusting CCM.

Announcing to the final results by Busanda Returning Officer Mr Dan Mollel, the winner was CCM’s candidates Ms. Leonsia Bukwimba who garnered 29,242 votes against her immediate opponent Chadema’s Mr Finias Magessa who scooped 22,799 votes.

Other candidates with the names of their parties in brackets are Mr Oscar Ndalawa (CUF) and Mrs. Beatrice Lubambe (UDP) scooped 957 and 271 votes respectively.

Tuesday, May 5, 2009

NYANGUMI NA PAPA WOTE WEZI, 'PUMBAVU ZENU'


Miezi mingi iliyopita niliwahi kusikia Mbunge mmoja akiongea kwenye mkutano wa bunge kuwa watanzania wote ni mafisadi,kauli hiyo ilimkosesha raha Spika Sitta na kumtaka mbunge huyo aliombe radhi bunge kwani akisema watanzania wote ni wezi basi hata rais pamoja na waheshimiwa wabunge ni wezi pia.


Lakini ukweli mni upi basi,hivi karibuni tumesikia minong'ono mikubwa inayomhusu mfanyabiashara maarufu nchini Reginald Mengi pamoja na mbunge Rostam Azizi.
Mengi anadai kuwa Rostamu ni Fisadi Papa, akimaanisha kuwa amekubuhu katika kufisadi mali za umma ikiwa ni pamoja na kujilimbikizia mali isivyo halali.
lakini naye Rostam akukaa kimya ameibuka na kudai kuwa Mengi ni nyangumi wa ufisadi, hivi ni vichekesho sana nadhani hawa mabwana wote wawili hawana maana ila wote wanapiga kelele kwa maana ya kutajka kujisafisha maovu yao.
Kinachofanyika hapa ni kila mmoja anatafuta nguvu ya kijamii, nadhani muda wenu ungalipo bado kitambo kidogo tu maovu yenu yatakuwa peupe,Ingelikuwa vyema mkakimbilia Yordan mkaoge ili mtakasike na kuwekwa huru na laana hii ya ufisadi.
Ninacho jua mimi mlevi hawezi kumtukana mtu safi ila mtu humtukana mlevi mwenzake, kadhalika fisadi hawezi kurushiana maneno na mtu asiye nacho bali fisadi kwa fisadi ukiwaweka pamoja watagombana tu, Mbona mnasahau elimu ya sumaku always negative na positive zinashabihiana lakini Positive kwa positive du!!,

Hongereni form 'Six', BIla kuboresha mazingira ya walimu haiwezekani

Mapema wiki iliyopita matokeo ya kidato cha sita yaliweza kutangazwa na na Baraza la mitihani la Tanzania - NECTA sambamba na hilo pia baraza hilo lilitangaza matokeo ya stashahada ya ualimu iliyofanyika mwezi wa pili, mwaka huu

Katika hali ya kusikitisha imeonyesha kuwa kiwango cha kufaulu kikishuka kwa wastani wa asilimia sita nukta moja ikilinganishwa na mwaka jana.
Kwa mujibu wa taarifa ya katibu mtendaji wa baraza hilo DK Joyce Ndalichako, watahiniwa 29,239 sawa na asilimia 87.21 ya waliofanya mtihani huo wamefaulu mwaka huu ambapo waliofaulu mtihani huo mwaka jana walikuwa sawa na asilimia 93.31 ya watahiniwa.

Sekondari ya wasichana ya Kifungilo imeongoza katika kundi la shule zenye watahiniwa zaidi ya 25, ikifuatiwa na shule ya wasichana ya Mpanda, Seminari ya Mtakatifu James, sekondari ya Changarawe na sekondari ya Nyerere - Migori wakati shule zilizofanya vibaya katika kundi hilo ni Lake, Ifunda - wasichana, Maswa, Zanzibar Commercial, Lumumba, Hamamnii na ufundi Ifunda.
Nadhani kuna kila haja kwa Wizara husika ikishirikiana na wataalamu wake kuhakikisha kuwa inapambanua chanzo kilicho sibu wanafunzi mwaka huu kushuka kiwango cha ufaulu badala yan kuendelea kupanda.
Lakini ninachoweza kushauri ni kwamba elimu nchini haitaweza kubadilika kama walimu wakiendelea kudharauliwa na kupewa ujira mdogo ambao unawashawishi kubuni mambo yao mengine ya kuweza kuwaingizia kipato na kuacha kabisa kuzingatia kuhusu taaluma yao ya kufundisha.

Friday, May 1, 2009

Jiji la Dar es Salam matatani


Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete akiangalia athari za mabomu yaliyotokea katika kambi ya jeshi eneo la Mbagala jijini Dar es Salaam.


Monday, March 16, 2009

Rais Kikwete tunasubiri asali ya London


Mapema siku ya jana Rais Jakaya kikwete aliondoka nchini yeye na wajumbe kadhaa kwa lengo la kuhudhuria mkutano mkubwa wa G-20 utakaofanyika nchini Uingereza katika jiji la London.

Wapo watu wengi wanaohoji kuhusu umuhimu wa safari hizo za rais kama ni bora na zinamanufaa kwa uchumi wa taifa hili changa.Pengine wamesahau uule usemi unaosema ndondondo si chururu

Katika hali hii wasomi na wadau mbalimbali wamediliki hata kueleza kuwa ni vema rais akapunguziwa ziara za kutoka nje kwani zinakuwa zikitumia mabilioni ya fedha ambazo zingetumika katika kutafuta pembejeo za kilimo na kununua madawa ya hospitalini.

Huu ni ukweli kabisa kwamba safari hizi zinapunguza kwa kiasi fulani pato la taifa kwa kuoneza matumizi,lakini cha kujiuliza ni je Taifa h ili linauwezo wa kusimama kwa miguu yake bila kupata misaada kutoka kwa wahisani.

Lakini pia fedha za kilimo na mambo mengi zinatokana na wahisani, je ni nani aliyezishughulikia au zilishuka kama mana jangwani.ya ‘Mungu mengi’ huu ni unafiki mkubwa wa baadhi ya viongozi na wasomi wanosema kuwa safari hizo hazina ulazima wowote

Tumeshughudia ziara nyingi anazofanya raisi katika nchi mbalimbali zikileta mafanikio kwa Tanzanuia, mambo haya ni pamoja na kufutiwa madeni na kupewa mikopo nafuu ambayo hadi hivi leo imekuwa suluhisho la baadhi ya kero za wananchi.

Mimi ninaamini kabisa kuwa Rais Kikwete ni mwadilifu na mchapakazi hodari hivyo anapoamua kulivalia njuga suala fulani hulitizama kwa pande zote , yaani kwa kuangalia faida na hasara zake.

Hivyo ni vema rais akaendelea kufanya safari zake nje ya nchi kwa kwenda mbele kwani watanzania tunaona matunda yake kila kunaopoitwa leo.

Amby.

Thursday, February 12, 2009

MPIJI-MAGOHE NA CHANGAMOTO TISA


Shule ya sekondari ya Mpji-magohe ni miongoni mwa shule za Serikali za kata ililyoanzishwa mwaka 2006 na hadi hivi sasa ina jumla ya wanafunzi 829 kutoka kidato cha kwanza hadi cha nne, ambapo wasichana ni 410 na wavulana ni 410.

Mpji magohe ni shule iliyopo umbali wa 10 km kutoka katika barabara kuu ya Morogoro jijini Dar es salaam

Shule hii mbali na kufanya vizuri kiasi katika elimu imekuwa ikikabiliwa na matatizo chungu mzima kama vile kukosekana kwa usafiri wa uhakika toka mbezi hadi mpiji kwa kuwa wanafunzi wengi makazi yao ni katika mji mdogo wa Mbezi jijini hapa.

Miongoni mwa kero zinazosababisha kutolewa kwa elimu chini ya kiwango ni pamoja na kuwepo kwa uhaba wa walimu wa sayansi na Hisabati, Uhaba wa vitabu vya kufundishia na maktaba, kukosekana kwa maabara ya utekelezaji wa masomo kwa njia ya vitendo.

Mkuu wa shule hiyo Bagaya Kashato anasema mbali na changamoto hizo pia kukosekana kwa maji na umeme pia kunachangia kwa njia moja au nyingine kupoteza muelekeo wa jitihada za wanafunzi katika kuhakikisha kuwa wanafanya vizurio katika mitihani yao.

Anasema nyumba za walimu nazo pia zimetoa mwanya wa kwa wanafunzi kindwa madarasani, ukiachilia mbali uhaba wa thamani kwa waalimu na wanafunzi.

Anasema edapo Serikali ikifanya jitihada za kuhakikisha inaondoa sehemu ya kero huizo katika shule za kati basi elimu itakayo kuwa inatolewa itazingatia vigezo vyote vya kitaaluma.

By Prince P

Tuesday, February 10, 2009

RAIS KIKWETE HAPO BRAVO

Ni vema na haki kusifu ama kupongeza jambo zuri linapofanywa na viongozi wetu wa serikali kijamii, kisiasa na hata kitamaduni.

Mambo haya hakika mbali na kuhamasisha jamii yanaleta uamsho ama morari wa kuongeza nguvu katika jambo fulani.

Mapema siku ya jana Rais Jakaya Kikwete aliweza kuongea na wachezaji wa timu ya Taifa Stars katika eneo la ikulu na kisha kuwatia moyo katika safari yao ya fainali za kombe la CHAN linalowahusisha wachezaji wanaocheza ligi za ndani.

Akizungumza nao aliwaeleza nini wanachotakiwa kukufanya kwa timu hiyo akidai “Watanzania tunataka raha, tupeni raha jamani” alisisitiza kikwete, huku akipokewa na sauti zilizosikika kuwa hatutakuangusha tutapigana kufa na kupona kulinda heshima ya taifa

Mfano huu wa rais Kikwete hakika ni wa kuigwa kwa asilimia kubwa kwani viongozi wengibne wakifanya jambo hili maendeleo katika jamii yanaweza kuonekana kwa kasi kubwa hapa nchini.
Peter.

Saturday, February 7, 2009

Kilichotokea Dodoma ni kizungumkuti


Mapema juzi tumeuhudia jambo ambalo baadhi ya vyombo vya habari vimeweza kuliripoti kinagaubaga nikiwa namaanisha ku waandishi waliweza kulitukuza na kuliandika kuwa Dk Slaa atumiwa majasusi, wengine ategewa vinasa sauti, wengine wakieleza kuwa amepangiwa njama za kumuangamiza kabisa kisiasa.

Hiki ni kitendawili kwa kweli, jambo hili ni wizi mtupu, kwani ukijaribu kwenda mbele na kurudi nyuma utagundua kuwa mambo mengi yasiyokuwa na msingi huwa yanatokea katika kipindi cha bunge hasa mahali ambapo mada ngumu zinapokuwa zikihadiliwa.
Nasema huu ni wizi mtupu ni vema wahusika wakagundua kuwa njama hizo za kulipua mambo ili tu kuwapoteza malengo wananchi ambao wanafuatilia kwa umakini shughuli za bunge zimepitwa na wakati, badala yake wanatakiwa kfikiri mbinu zingine za kuwapoteza maboya wananchi.

Mimi nataka kufahamu, kuna mambo mengi mazuri yaliyokuwa yakiendelea bungeni lakini kutokana na kutokea kwa jambo hilo vyombo vya habari vilisahau kuyapa kipaombele mambo ambayo kwa namna moja au nyingine ni sehemu ya kuondokana kwa umaskini kwa mtanzania wa hali ya chini kabisa.

“huu ni wizi,tena wizi mtupu ni vema watu wakafungua macho na kuangalia mbele ili waone” ushauri wangu kwa watanzania ni kuhakikisha kuwa jambo hilo la Slaa na mwenzake halipewi kipaombele bali warudi nyuma na kuyaangalia mambo yao waliyokuwa wakiyafuatilia bungeni.

Mguso

Friday, February 6, 2009

WE HAVE KNOWLEDGE, LET US USE IT

As I said earlier internet will remain to be basic tool in our day to day life of journalism, No matter on the way it function but what is important is what we used to get in this tool. Bay the way we found many fact information by visiting different links.

It is now five day since we have started this internet workshop. We used to pass through different topic like how Internet has changed society and communication globally, Journalism in the age of internet, the use of internet in every day journalism.

Others topic are like African and international web resource, finding information to the Website, Email communication skills, Plagiarism and copy white where by our Trainer Johansson tells about the ethics of copy and paste date from the web site.

But also we used to see how Blogs function and how to pass through in it , in the topic which said Blogs and Citizen Journalism. Each participant in this session achieve to open their blog like mine (maishanyundo.blogspot.com.
I can say it was real enjoyable session from the time we start until the end of this workshop. I my self I gain more things which will help my company in one way or another .

I’m quit sure that in this time of global change we journalist suppose to know in deeply about the uses of internet in our daily activities .My experience is that, many journalist when they failed to find some information from the source they live stories, but instead they can use also Internet to search for they are news information.

I cant say I don’t get anything in this workshop, instead of enjoying in each and every thing but also I get good material and basic knowledge to boost up my experience, which was my vision in this work shop.

God bless Peik Johansson and MISA Tanzania too.

Thank you.

TUKUBALI MABADILIKO

Katika matumizi ya kila siku kumekuwep[o na ongezeko makubwa la matumizi ya mtandao kila kukicha jambo ambalo linasadikiwa kuwa huifanya dunia iweze kubebwa katika viganja vya kila mtu.
Tunashuhudia mawasiliano mya kitekinolojia yakiongezeka kila kunapoitwa leo kwani jambo linalotendeka hivi leo katika nchi ya Marekani kadhalika na hapa pia nchini linaweza kuonekana kwa urahisi kabisa.

Hivi karibuni tulishuhudia kuapishwa kwa raisi Barack Obama ambapo kwa muda mmoja dunia iliweza kushuhudia kwa wakati mmoja kuapishwa kwake, Thats why nasema bado kitambo kidogo sana dunia itakuwa karibu kupindukia.

Utaungana nami kuwa ili kuleta mabadiliko ya kitekinolojia kwa vizazi vijavyo sisi tuliopo hatuna budi kushinikiza elimu hii ya Mtandao wa komputa( Internet) ikiwa endelevu kuanzia katika shule za msingi ili mabadiliko haya yasituache nyuma sana.

Tunafahamu Sasa

Waandishi wa habari wakishiriki katika mafunzo ya matumizi ya mtandao(Internet) kwa maisha ya kila siku ya kiuandishi





Thursday, February 5, 2009

INTERNET BRINGS THE WORLD TOGETHER

It was good day for me, we start the lesson at early time, I mean in ample time as we are. We used to do many thing in this day relating to the internet in every day journalism,among those essues is like perusing material, searching for currency, time table, football games.

Our trainer Johansson put in the picture the meaning of internet to our day life in this field of reporting. He says Internet is a global system of interconnected computer network that interchange data and gives out different fact and information accordingly .

Apart from that we used to follow up different links which can support us in our day to day activities. For example we search for uefa in this engine we see different material of sports, This web sustain the sport reporter to gain different material so that they can come up with good fact and back ground of any sport issues.

Also we pass through the government web page and find many data which can support our work, this engine is Tanzania we used to see data like Ruvuma population, and many this facing our work.

It is true that, we journalist we are supposed to to know each other concerning the Internet in our daily , so au to cover and see about millions document of private and public, academic, business, and government networks of local to global scope that are linked also it carries various information and services.

Thank You

Tuesday, February 3, 2009

Journalism in the age of internet

It was so fantastic day , because we used to hire and knowing each other coming from out trainer. Even though our today topic was based in ‘ Journalism in the age of Internet ‘ we used to persuade in learning on how to open the blog.

What is interesting is about the topic, what i think is The daily newspaper industry is especially in danger by the internet. Though many news paper are continue to be registered.

Now days we see many young generation used to find fact on the Internet rather than in the news paper. It is like an alarm which express the deadly of print media but not surely. many of them visit Google News several times a day to get the latest. Information on the world.

According to Rupert Murdoch to the American Society shows his interest of media to connect them self into internet system if they want to do good. I can not say by the way but my point is in this world of global information our media suppose to jump themselves to this category if they want to make it.

But it is something which can come up slowly in those un-developed country because always challenge are there.

I say this will come slowly in un developed country, because a great newspapers hire in Tanzania and also in Africa ,the computer technology in the newsroom was hopelessly out of date as the paper didn’t have the money to invest in new technology.

So i sought the better ways to live in the internet age, first in the form of requiring payment for access to its web site, more recently by providing such access for free.

Thank you

Internate Workshop


Name: Peter Edson
Occupation: Journalist
Working place: Mwananchi Communication Ltd
Job Title: Reporter/ Web Content Developer

I’m proud to be among the participant who participate in Internet workshop for editor and Trainers, organized by MISA- Tanzania and VIKES foundation center.

I’m real enjoying because i used to know more about different issues which I never taught before. Apart from that, our trainer Peik Johansson instruct us about different ways of finding the fact in internet in this period of modernize journalism , it was agreeable .

My expectation on other days coming I wish I can learn more about the uses of internet for the purpose of being a good ambassador for internet uses

All the best